Tafauti Kati ya hadithi fupi na riwaya

Tofauti kati ya hadithi fupi na riwaya
Zipo tofauti mbalimbali zinazojitokeza kati ya utanzu wa hadithi fupi na utanzu wa riwaya.Miongoni mwa tofauti hizo ni kama zifuatazo:
Tofauti ya upana wa  mawanda:riwaya hutumia mawanda mapana kwani kila jambo hupewa uzito wake na kuelezwa kwa mapana ya kutosha lakini hadithi fupi mambo yake huelezwa kwa ufupi na mkato tu.
Tofauti ya wahusika:Riwaya hutumia wahusika wengi na wahusika hao huelezwa kiurefu,riwaya pia huhusisha mhusika mkuu na wahusika wasaidizi lakini hadithi fupi huwa na wahusika ambao huwa hawaelezwi kwa urefu ukilinganisha na wahusika wa riwaya.
Tofauti ya urefu:Riwaya ni kazi yakubuni ambayo ni ndefu urefu wake unatokana na uchangamano wa visa na wahusika wengi lakini hadithi fupi ni kazi ya sanaa ambayo ni fupi kiasi kwamba inaweza kusomwa kwa kikao kimoja na kumaliza.
Tofauti ya uchangamano:Riwaya ina muundo changamano kutokana na wingi wa matukio lakini hadithi fupi ina muundo sahili usiochangamana kwani hadithi fupi hueleza juu ya tukio moja tu.
Tofauti ya dhamira:kikawaida riwaya huwa na dhamira kuu na dhamira ndogondogo lakini hadithi fupi huwa na dhamira chache wakati mwingine huwa na dhamira moja tu.

No comments:

Post a Comment

UTUNGAJI WA KAZI ZA FASIHI ANDISHI Utungaji wa kazi za fasihi andishi nii mada inayogusa au inayohusu ubunifu wa maandishi. Kubuni ni kutn...