Muundo wa Tamthiliya

Vipengele/Muundo wa Tamthiliya
Hadithi(Simulizi):Huwa ni kisa cha kubuni au cha kweli au mchanganyiko wa vyote viwili,hadithi huwa na mzozo Fulani wa pande mbili hadi kufikia mwisho wake. AB- chanzo au mwanzo wa mchezo, chanzo cha mgogoro huelezwa na tamthiliya kama ni hali ya majonzi au furaha, wakati na mahali panapotokea vitendo vya hadithi wahusika hutambulishwa. BC- kukua kwa mgogoro,mvutano baina ya pande mbili  hujitokeza chanzo cha mgogoro huelezwa, njia za kutatua tatizo na kujaribu kutatua tatizo hilo. C- tatizo limefika kileleni ambapo uwezekano wa kulitatua huwa haupo. CD- mgogoro huanza kuleta mshtuko na taharuki hutokea. DE- mgogoro hufika mwisho.
Vitendo:Tamthiliya hugawanyika katika sehemu kuu ziitwazo vitendo. Kila kitendo huzingatia tendo moja kuu,tamthiliya huwa na vitendo vitano,vitendo hugawanyika katika sehemu ndogondogo ambazo ni maonyesho ambapo onyesho moja huwa na tukio moja linalotendeka mahala pamoja, onyesho moja hutenganishwa na onyesho jengine kutegemea na kitu kinachosimuliwa, kumalizika kwa tukio huashiria wahusika kuondoka, kuzima taa nakadhalika.
Wahusika:Ni viumbe hai wanaobebeshwa matendo ya mwanadamu katika kazi ya fasihi, uhusika wao huhusiana na kile wanachokizungumzia, na pia wahusika wake hawatofautiani na wahusika wa hadithi wa hadithi ambapo kuna wahusika wakuu na wahusika wadogo.
Dayalojia:Ni Mazungumzo/majibizano baina ya wahusika .Kufanikiwa kwa msanii kutategemea ni jinsi gani anatunga dayalojia yake kwa namna ya kuvutia na azingatie maneno machache yanayojitosheleza, pia monolojia huwerza kutumika pale ambapo mhusika anakuwa anawaza mwenyewe moyoni.
Mbinu nyengine:Pia msanii wa tamthiliya anaweza kutumia mbinu mbalimbali ili kuipamba na kuifanya tamthiliya yake ivutie kwa hadhira na hatimaye kuweza kuibua dhamira lengwa kwa jamii,baadhi ya mbinu hizo ni kama matumizi ya mbinu ya utambaji,ngano nakadhalika.

No comments:

Post a Comment

UTUNGAJI WA KAZI ZA FASIHI ANDISHI Utungaji wa kazi za fasihi andishi nii mada inayogusa au inayohusu ubunifu wa maandishi. Kubuni ni kutn...