Mambo muhimu ya kuzingatia katika utunzi wa hadithi

Mambo muhimu ya kuzingatia katika utunzi wa hadithi
Maudhui:mwandishi ana uhuru wa kuandika kitu chochote ambacho kina manufaa kwa jamii na umma kwa ujumla pia maudhui ya hadithi hutofautiana toka jamii moja na nyingine na hutofautiana na mazingira na mahitaji ya jamii hiyo.hadithi hujengwa na dhamira kuu na dhamira ndogo ndogo
Muundo wa hadithi:Muundo ni mpangilio wa visa na matukio katika kazi ya fasihi andishi.Mtunzi mzuri ni Yule anaejua kupangilia visa na matukio na kusuka visa vyake kwa umakini zaidi kiasi cha kumvutia msomaji wake awe na shauku ya kuendelea kusoma kazi hiyo ya fasihi. Mara nyingi hadithi huwa na muundo wa msago, riwaya huwa na muundo wa rukia na msago.
Mtindo wa kazi:Kazi iliyo nzuri mara nyinmgi huwa na vionjo kwa msomaji, msanii inabidi atumie mbinu mbali mbali za kumvutia msomaji kwani msanii anaweza kutumia mbinu za fasihi simulizi pia anaweza kuchanganya tanzu za fasihi katika tanzu yake hiyo.Pia monolojia na dayalojia.
Matumizi ya lugha:Lugha ndio nyenzo kuu ya kazi yoyote ya fasihi,kwani kwa kiasi kikubwa lugha husaidia katika kuunda fani na maudhui ya kazi ya fasihi.Ni vyema mtunzi akitumia lugha yenye vionjo ili kuweza kuwa na umakini kwa msomaji .halikadhalika msanii inabidi atumie usanii katika kuweza kumpa kila mhusika na lugha yake ili imsaidie katika kutambulisha mhusika wa kazi hiyo pia lugha yake iwe inaendana na wasifu wa mhusika wa kazi hiyo.Vilevile lugha iwe na tamathali za semi kama vile sitiari,tafsida,tanakali sauti,tashbiha,tashhisi lugha ya taswira na mbinu nyengine za kisanaa
Uteuzi na uumbaji wa wahusika:Mwandishi anapswa kuchagua na kuumba wahusika wake kiasi cha kukubalika na hali halisi kitabia na maumbile.Mfano kama mhusika ni kiongozi basi aonekane ni kiongozi kweli.Riwaya huwa na wahusika wakuu na wahusika wasaidizi wote hujengwa na kuelezwa kiurefu.
Uteuzi wa jina la kitabu(Hadithi):Msanii anapaswa kuwa makini katika kubuni jina la kitabu kwa sababu jina ndilo linalomvutia msomaji ,vilevile msanii anapaswa kuzingatia katika kubuni jina hilo kwani jina la kitabu linapawa liendane na maudhui yaliyomo ndani ya hadithi hiyo.
Uteuzi wa mandhari:Mandhari ni sehemu au mahali ambamo kazi ya fasihi inafanyika.Ujenzi mbaya wa mandhari huleta athari mbalimbali katika hadithi na riwaya.Kuna mandhari za aina mbili ambazo ni mandhari ya kubuni na mandhari halisi. Vilevile mandhari yakielezwa vizuri huimarisha mfumo wa hadithi/riwaya pamoja na ujengaji wa wahusika wake.Mandhari ikiibuliwa vibaya huathiri mfumo mzima wa kazi ya fasihi ,pia matumizi ya vifaa viendane na wakati.

No comments:

Post a Comment

UTUNGAJI WA KAZI ZA FASIHI ANDISHI Utungaji wa kazi za fasihi andishi nii mada inayogusa au inayohusu ubunifu wa maandishi. Kubuni ni kutn...